JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MSULUHISHI WA MIGOGORO YA BIMA

TIRA Logo
Rais Samia Awahimiza Watunza Kumbukumbu Kuzingatia Usiri.
27 Nov, 2022
Rais Samia Awahimiza Watunza Kumbukumbu Kuzingatia Usiri.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza watunza kumbukumbu kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo ya kiutendaji ndani na nje ya Serikali.

Rais Samia ametoa agizo hilo leo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 10 wa Chama cha Taaluma ya Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) katika Ukumbi wa Mikutano wa AICC.

Aidha, Rais Samia amewataka watunza kumbukumbu na nyaraka katika ofisi za umma kutunza siri za Serikali kwa kusimamia maadili ya kazi yao ili kulinda usalama wa nchi.

Vile vile, Rais Samia ametoa wito kwa waajiri Serikalini na sekta binafsi kuhimiza matumizi ya teknolojia kwenye utunzaji wa kumbukumbu na kuimarisha mazingira ya kazi kwa kupunguza mrundikano katika vyumba vya masijala.

Hali kadhalika, Rais Samia amesema matumizi ya teknolojia katika utunzaji wa kumbukumbu utasaidia kurahisisha upatikanaji taarifa zinapohitajika kwa ajili ya maamuzi mbalimbali.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza watunza kumbukumbu kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo ya kiutendaji ndani na nje ya Serikali.

Rais Samia ametoa agizo hilo leo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 10 wa Chama cha Taaluma ya Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) katika Ukumbi wa Mikutano wa AICC.

Aidha, Rais Samia amewataka watunza kumbukumbu na nyaraka katika ofisi za umma kutunza siri za Serikali kwa kusimamia maadili ya kazi yao ili kulinda usalama wa nchi.

Vile vile, Rais Samia ametoa wito kwa waajiri Serikalini na sekta binafsi kuhimiza matumizi ya teknolojia kwenye utunzaji wa kumbukumbu na kuimarisha mazingira ya kazi kwa kupunguza mrundikano katika vyumba vya masijala.

Hali kadhalika, Rais Samia amesema matumizi ya teknolojia katika utunzaji wa kumbukumbu utasaidia kurahisisha upatikanaji taarifa zinapohitajika kwa ajili ya maamuzi mbalimbali.